DARASA LA SABA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KUDATO CHA KWANZA 2016/2017

Kujiunga kidato cha kwanza Tanzania

Kujiunga kidato cha kwanza 

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA  KUDATO CHA KWANZA 2018/2019, FORM ONE SELECTION 2018/2019, SELECTION DARASA LA SABA 2016/2017.

waliochaguliwa kidato cha kwanza 2018/2019

WE WISH YOU A MERRY XMASS! - ALL THE STUDENTS!

majina ya waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2019

 

Jafo atangaza waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2019 Leo tarehe 13/12/2018 - Form One Selection 2019 - New Updates


Serikali yatangaza majina ya waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018.


Wanafunzi 650,862 kati ya 662,035 waliofaulu wamechaguliwa katika awamu ya kwanza, hii ikiwa ni sawa na asilimia 98.31

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo amesema  kati ya wanafunzi 662,035 waliofaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi  wanafunzi  650,862 sawa na asilimia 98.31 wamechaguliwa  kujiunga na  masomo ya kidato cha  kwanza katika awamu ya kwanza  mwaka 2018

Akitangaza matokeo ya uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018  idadi ya wanafunzi   mwaka huu imeongezeka  kwa wanafunzi 124,209 ambapo ni sawa na asilimia  23.58 ikilinganishwa na wanafunzi 526,653 waliochaguliwa awamu ya kwanza kuingia kidato cha kwanza mwaka 2017.

Wanafunzi 1912 wenye uhitaji maalum (pupils with special needs) waliofaulu mitihani ya darasa la saba  wamechaguliwa  kujiunga  na masomo ya kidato cha kwanza mwaka 2018 kwenye shule za sekondari za Serikali.

Mhe. Jafo amefafanua kuwa wanafunzi  11,173 sawa na asilimia 1.69 ya waliofaulu hawakupata nafasi ya kuchaguliwa  kujiunga  na kidato cha kwanza katika awamu ya kwanza  ya uchaguzi  kutokana na uhaba  wa miundombinu ya elimu hususani  vyumba vya madarasa kwenye baadhi ya Halmashauri.

Halmashauri ambazo zimeshindwa kuwapangia wanafunzi wote waliofaulu nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza ni Halmashauri za Lindi wanafunzi (80) Mbeya (207),Halmashauri ya  Jiji la Mbeya  ( 1,227), Mbarali (1,578),  Kalambo (166), Nkasi (1,318), Halmashauri ya Wilaya ya  Sumbawanga (1,054), Halmashauri ya Manispaa  ya Sumbawanga (1,553), Babati (581). Hanang (687), Mpanda (262), Nsimbo (714), Halmashauri ya Mji wa Bariadi (369) na Halmashauri ya Wilaya ya Busega (1,207).

Mhe. Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa ambayo haijakamilisha ujenzi wa miundombinu hasa ya vyumba vya madarasa  kuhakikisha wanakamilisha hadi kufikia mwezi februari, 2018 ili wanafunzi watakaochaguliwa kwenye awamu ya pili wapate nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018.

“Lengo la Serikali  ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliofaulu mtihani wa darasa la saba wanapata nafasi  ya kujiunga  na masomo ya kidato cha kwanza  maelekezo  yametolewa kwa wakuu wa mikoa kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanapata nafasi  ya kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2018” Amesema Jafo



shule walizopangiwa kidato cha kwanza 2018 (Video)

 

WHAT DOES IT TAKE TO BECOME A SUCCESSFUL STUDENT?

 

Darasa la Saba waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2017.

 

Matokeo Yote Ya Mitihani - One Spot For All The Examination Results

Selection kidato cha kwanza 2017


Biology Lessons & Notes - FORMS I, II, III, IV

 

94.8% Wachaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2017

WANAFUNZI 526,653 sawa na asilimia 94.8 ya waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwakani katika shule za sekondari za serikali katika awamu ya kwanza huku 28,638 wakishindwa kupangiwa shule katika awamu ya kwanza.

Kati ya wanafunzi hao, wasichana ni 268,052 sawa na asilimia 94.5 ya wasichana waliofaulu na wavulana ni 258,601 sawa na asilimia 95.2 ya wavulana waliofaulu. Wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka 2016 walikuwa 795,739, huku 244 wakifutiwa matokeo ya mtihani kutokana na udanganyifu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene alisema wanafunzi waliochaguliwa wamegawanyika katika makundi manne likiwemo:-
  • Shule za bweni kwa wenye ufaulu mzuri ambao waliochaguliwa ni 900 wavulana 480 na wasichana 420.
  • Shule za bweni za ufundi waliochaguliwa - 1,005.
  • Shule za bweni kawaida - 780.
  • Shule za bweni kwa wenye ulemavu - 723.
  • Shule za kutwa wanafunzi waliochaguliwa - 523,245. 
Jumla ya wanafunzi 3,408 sawa na asilimia 0.6 wamechaguliwa kwenda sekondari za bweni na jumla ya watahiniwa 555,291 walifaulu sawa na asilimia 70.36 ya wanafunzi waliofanya mtihani, kati yao wasichana ni 238,753 sawa na asilimia 51.1 na wavulana 271,538 sawa na asilimia 48.9.

Ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 ukilinganisha na asilimia 67.84 kwa mwaka 2015.

Simbachawene alisema katika uchaguzi huo, wanafunzi 28,638 hawakuchaguliwa katika awamu ya kwanza, na kuitaja mikoa ambayo wanafunzi wamebaki ni Dar es Salaam (18,820), Arusha (4,752), Songwe (1,465), Kigoma (1,208), Manyara (1,141), Lindi (608), Mbeya (406) na Katavi (238).

Aidha, waziri huyo alisema kati ya wanafunzi 1,060,588 walioanza darasa la kwanza 2010, wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka 2016 ni 795,739 sawa na asilimia 75 ya wanafunzi walioandikishwa wakiwemo wasichana 422,562 sawa na asilimia 53.1 na wavulana 373,177 sawa na asilimia 46.9 ya waliosajiliwa.

Akizungumzia udanganyifu, alisema watawavua madaraka kwa waliokuwa waratibu elimu kata na walimu wakuu, kuwashitaki mahakamani na kupeleka mashauri yao Tume ya Utumishi ya Walimu, baada ya udanganyifu kuongezeka ambako watahiniwa 244 wamefutiwa matokeo mwaka 2016 ikilinganishwa na wanane wa mwaka jana.

SUCCESS JOURNEY - What Most Successful people do.

 Alizitaja shule zilizohusika kwenye udanganyifu huo ni Shule ya Tumaini na Little Flower za Sengerema mkoani Mwanza, Mikahamakumi iliyopo Sikonge, Tabora ambazo ni za binafsi, wakati za serikali ni Kondi Kasandalala iliyopo Sikonge, Tabora, Qash iliyopo Babati na St Getrude iliyopo Madaba mkoani Ruvuma.

Aidha, alisema 10 bora za serikali ni Kazunzu iliyopo Halmashauri ya Buchosa (Mwanza), Mwanahegele ya Maswa (Simiyu), Huruma ya Mbinga (Ruvuma), Kabanga ya Ngara (Kagera), Butumba B (Jiji Mwanza), Masoko ya Kilwa (Lindi), Lyambamgongo ya Bukombe (Geita), Kilimani ya Geita Vijijini, Magufuli ya Chato na Nkome ya Geita Vijijini, Geita.

Alisema shule 10 zilizofanya vibaya ni Chohelo ya Mvomero (Morogoro), ambayo ni ya mwisho kitaifa ikifuatiwa na shule za Iloliento, Longido (Arusha), Mwalebi na Nchilila Meatu (Simiyu), Magingi ya Mvomero, Kilole ya Lushoto, Tanga, Zege ya Korogwe, Tanga na shule tatu za Lubchi, Kitengo na Mgata za Morogoro vijijini.

waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2018

PAST PAPERS FOR RIVISION / Form two past papers, Form four past paper, Form six past papers (Rivision Made Simple!) - New



TIPS FOR STUDYING

 

THE MAGIC  POWER OF A SMILE!


How to celebrate a New Year 2017

 

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SEKONDARI 2016/2017, DARASA LA SABA WALIOCHAGULIWA KWENDA SEKONDARI 2016/2017, KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2016/2017, KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA. 

waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2018

DARASA LA SABA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KUDATO CHA KWANZA 2017/2018

FORM ONE SELECTION 2017/2018, SELECTION DARASA LA SABA 2017/2018.

 

shule walizopangiwa kidato cha kwanza 2017


Form one selection 2017 Kenya.