WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI MWAKA 2015 WALIOBADILISHIWA SHULE/TAHASUSI

MABADILIKO YA SHULE/TAHASUSI KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI MWAKA 2015

Ofisi  ya  Waziri  Mkuu  Tawala  za  Mikoa  na  Serikali  za  Mitaa  (OWM- TAMISEMI)  ilitangaza  majina  ya  wanafunzi  wa  kujiunga  na  Kidato  cha Tano  na  Vyuo  vya  Ufundi  mwaka  2015,  tarehe  30  Juni,  2015.  Baada  ya majina  haya  kutangazwa,  OWM-TAMISEMI  imepokea  maombi  mengi toka  kwa  Wazazi/Walezi  na  Wanafunzi  ya  kuomba  kubadilishiwa  Shule na/au  Tahasusi  kutokana  na  sababu  mbalimbali.  OMW-TAMISEMI imeyachambua  maombi  haya  kwa  kuzingatia  sababu  zilizotolewa  na waombaji,  uwepo  wa  nafasi  kwenye  shule  walizomba  na  ufaulu  wa mwanafunzi aliyeomba kubadilisha tahasusi.

Kwa  wanafunzi  ambao  majina  yao  hayajaonekana  kwenye  orodha  hii  na wale  waliobadilishiwa  shule/tahasusi  mnahimizwa  kwenda  kuripoti kwenye  shule  mlizopangiwa  na  ikumbukwe  kuwa  tarehe  ya  mwisho  ya kuripoti  ni  tarehe  31  Julai,  2015.  Kushindwa  kufanya  hivyo,  nafasi  zao zitagawiwa kwa wanafunzi waliokosa nafasi.

Imetolewa na
KATIBU MKUU OWM-TAMISEMI

Bofia Hapa: ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI MWAKA 2015 WALIOBADILISHIWA SHULE/TAHASUSI

AU

Bofia Hapa: ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI MWAKA 2015 WALIOBADILISHIWA SHULE/TAHASUSI