Ratiba ya mtihani wa darasa la nne - SFNA Timetable 2019


RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA NNE 2019

RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (STANDARD FOUR NATIONAL ASSESSMENT TIMETABLE) NOVEMBA, 2019

SFNA TIMETABLE 2019

TAREHE NA SIKU  
MUDA (SAA) 
NAMBA MFICHO 
    SOMO
20.11.2019
JUMATANO
2:00-3:30 06
06E
URAIA NA MAADILI
CIVIC  AND MORAL EDUCATION
3:30-4:30 MAPUMZIKO
4:30-6:00 04
04E
HISABATI
MATHEMATICS
6:00-8:00 MAPUMZIKO
8:00-9:30 01 KISWAHILI




21.11.2019
ALHAMISI

4:30-6:00 05
05E
SAYANSI NA TEKNOLOJIA
SCIENCE AND TECHNOLOGY
6:00-8:00 MAPUMZIKO
8:00-9:30 03
03E
MAARIFA YA JAMII
 SOCIAL STUDIES

PATA MATOKEO YA DARASA LA nne 2018/2019 (SHULE ZA MSINGI) KIMKOA

MAELEKEZO MUHIMU
  1. Hakikisha kuwa unayo Ratiba ya Upimaji wa mwaka 2019 iliyoandaliwa na Baraza laMitihani la Tanzania.
  2. Kabla ya kufungua bahasha yoyote yenye maswali ya upimaji,  hakikisha kwambaunasoma jina la somo juu ya bahasha husika na kujihakikishia kuwa somo hilo ndilo linalostahili kufanyika wakati huo kulingana na Ratiba ya Upimaji.
  3. Endapo utata utajitokeza kati ya maelekezo yaliyomo ndani ya Karatasi ya Upimaji na Ratiba ya Upimaji, maelekezo yaliyomo katika karatasi ya upimaji husika ndiyo yatakayofuatwa.
  4. Wanafunzi WASIOONA na wale wenye UONI HAFIFU waongezewe MUDA WA ZIADA WA DAKIKA 10 KWA KILA SAA kwa upimaji wote isipokuwa  DAKIKA 20 KWA KILA SAA  kwa somo la Hisabati.
  5. Msimamizi wa Wanafunzi WASIOONA awe mtaalamu mwaminifu aliye na uwezo wa kusoma maandishi na alama za ‘Braille’.
  6. Wanafunzi wenye UONI HAFIFU wapewe karatasi za upimaji na za kujibia zenye maandishi yaliyokuzwa, zilizoandaliwa na Baraza la Mitihani la Tanzania kwa matumizi yao.
  7. Wanafunzi waelekezwe;
  • Kuingia ndani ya chumba cha upimaji nusu saa kabla ya muda  wa upimaji na watakaochelewa kwa zaidi ya nusu saa baada ya upimaji kuanza hawataruhusiwa. 
  • Kufuata maelekezo yote yatakayotolewa na wasimamizi wa upimaji.
  • Kuandika jina kamili na namba ya upimaji kwa usahihi.
  • Kutofanya mawasiliano ya maneno au kwa njia yoyote baina yao. Ikiwa mwanafunzi ana tatizo anatakiwa kunyoosha mkono ili kuomba msaada kwa msimamizi wa upimaji.
  • Wakijihusisha au wakifanya udanganyifu watafutiwa matokeo yao ya upimaji.