OTEAS Tamisemi - Nafasi za ajira za walimu

Ajira za ualimu Tamisemi>>ajira ya walimu 2020


NAFASI ZA AJIRA ZA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI. AJIRA ZA UALIMU

Ajira za walimu - OTEAS - Tamisemi

Ajiara za ualimu Tamisemi - OR-TAMISEMI inawatangazia walimu wenye sifa kutuma maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi cha ajira.tamisemi.go.tz - OnlineTeacher Employment Application System – OTEAS.
OTEAS - Ajira za walimu Dar es salaam Tanzania

Walimu wanaotakiwa kutuma maombi ni wenye sifa za kitaaluma kama ifuatavyo:

A. WALIMU WATAKAOAJIRIWA SHULE ZA MSINGI

  1. Mwalimu Daraja la IIIA - mwenye Astashahada (Cheti) ya Ualimu;
  2. Mwalimu Daraja la IIIB - mwenye Stashahada (Diploma ya Ualimu katika masomo ya English, Civics, Historia, Jiografia na Kiswahili;

B. WALIMU WATAKAOAJIRIWA SHULE ZA SEKONDARI

  1. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu waliosomea Elimu Maalum; 
  2. Mwalimu Daraja la IIIB - mwenye Stashahada (Diploma) ya Ualimu waliosomea Elimu Maalum;
  3. Mwalimu Daraja la IIIB - mwenye Stashahada ya Ualimu somo la Physics, Mathematics , Biology & Chemistry;
  4. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu somo la Agriculture Science;
  5. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu somo la Home Economics;
  6. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu somo la Physics, Mathematics, Chemistry & Biology;
  7. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu somo la Book Keeping, Commerce, Accounts & Economics; na
  8. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu somo la English, Civics & General Studies.
  9. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Mahitaji Maalum aliyehitimu Shahada ya Ualimu kwa masomo ya English, Civics, General Studies, History, Geography & Kiswahili.
  10. Mwalimu Daraja la IIIC - mwenye Shahada ya Ualimu kwa masomo ya English, Civics, General Studies, History, Geography & Kiswahili.

C. SIFA ZA JUMLA

Waombaji wa nafasi tajwa hapo juu wawe na sifa za jumla zifuatazo:-
  1. Awe ni Mtanzania;
  2. Awe amehitimu chuo kinachotambulika na Serikali kati ya mwaka 2014 hadi 2017; isipokuwa kwa wahitimu wa Elimu ya Ualimu wa masomo ya Fizikia na Hisabati;
  3. Asiwe na umri wa zaidi ya miaka arobaini na tano (45) wakati wa kutuma maombi haya;
  4. Walimu waliowahi kutuma maombi na hawajaajiriwa wanapaswa kutuma maombi upya.

D. MWISHO

Maombi yote yawasilishwe kwa mtandao na yawe na nakala za vyeti vya taaluma,utaalam na kuzaliwa. Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe 15/03/2019.

ONLINE TEACHERS APPLICATION SYSTEM -(OTEAS)

You have account >> OTEAS LOG IN


You don't have account create one here>>OTEAS Online Application


ajira mpya

ajira tanzania

ajira za afya

ajira za community health