HESLB - Bodi ya mikopo ya elimu ya juu

HESLB - MASWALI  NA  MAJIBU  21  YA  UTARATIBU,  SIFA  NA VIGEZO VYA UTOAJI MIKOPO KWA 2019/2020

BODI YA MIKOPO (HESLB) TANZANIA

heslb - Bodi ya mkopo 2019 - wanafunzi waliyopewa mikopo 2019/2020

TCU - List Of Universities (Vyuo Vikuu Tanzania) - New Updates

Zipi ni sifa kuu za kupata mkopo wa elimu ya juu?

  • Awe mtanzania
  • Awe ameomba mkopo kwa utaratibu ulioelekezwa (online)
  • Awe amepata udahili (admission) kwenye chuo kinachotambuliwa na jina lake kuwasilishwa Bodi ya Mikopo
  • Asiwe na chanzo kingine cha kugharamia masomo yake ya chuo kikuu (mfadhili, ZHELB n.k)
  • Maelezo ya kina kuhusu sifa na vigezo hutolewa na Mwongozo

Admission Guide Book 2019/2020 for Form Six Applicants

Admission Guide Book 2019/2020 for Ordinary Diploma/Equivalent Applicants

Ninapaswa kufanya nini ili niweze kuanza kuomba mkopo kwa njia ya mtandao (OLAMS)?

  • Soma  mwongozo  uliotolewa  na  Bodi  ambao  unapatikana  katika tovuti  ya  Bodi  (www.heslb.go.tz),  kisha,  fungua  mtandao  wa maombi (www.olas.heslb.go.tz) ili ujisajili kwa kutumia namba yako ya mtihani wa kidato cha nne na mwaka uliofanya mtihani huo.

Baada ya kujisajili, napaswa kufanya nini?

  • Baada  ya  kujisajili,  utapata  namba  ya  kumbukumbu  (Control Number) kwenye ‘screen’ ambayo itakuwezesha kufanya malipo ya ada ya maombi ya TZS 30,000/= kwa njia ya benki au simu. Lipa mara moja tu! Kiasi kamili cha TZS 30,000/=
  • Baada ya kulipa, utapokea ujumbe (sms) wa uthibitisho wa muamala wako utakaokuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ya maombi. Jaza hatua kwa hatua.

Ni nyaraka gani muhimu zinatakiwa wakati wa kuomba mkopo?

Nakala za:
  1. Cheti cha kuzaliwa cha mwombaji kilichothibitishwa na RITA
  2. Vyeti vya kidato cha IV & VI au Stashahada (Diploma)
  3. Cheti cha kifo ikiwa umepoteza mzazi kilichothibitishwa na RITA;
  4. Kitambulisho  cha  mdhamini  (NIDA,  Mpiga  Kura;  Leseni  ya Udereva au Pasi ya Kusafiria). Mdhamini anaweza kutumia kimoja kati ya vitambulisho hivi.
  5. Barua  ya  taasisi  mfadhili  (Sponsor)  ikiwa  ulifadhiliwa  katika masomo ya sekondari
  6. Barua ya Mganga Mkuu wa Wilaya au Mkoa ikiwa mwombaji au mzazi wake ana ulemavu
  7. Picha (passport size) za mwombaji wa mkopo na mdhamini wake (mdhamini anaweza kuwa mzazi au mlezi)

Je, iwapo nimehitimu kidato cha sita au diploma mwaka huu 2019 na sijapata cheti nitaambatanisha nini?

  • Unatakiwa  kujaza  namba  ya  mtihani  wa  kidato  cha  sita  ambayo itaweza  kuhakikiwa  na  mamlaka  husika.  Kwa  mhitimu  wa  diploma (Stashahada),  unaweza  kuambatanisha  waraka  wa  matokeo (transcript).

Je, mwanafunzi anaweza kupata usaidizi wa kuomba mkopo kwenye ‘Internet CafĂ©’?

  • Ndio.  Hata  hivyo,  unashauriwa  kuhakikisha  kuwa  taarifa  zako zimejazwa kwa usahihi. Hakikisha viambatanisho vyote (vyeti, barua n.k) vimewekwa/vimepakiwa kwenye fomu yako mtandaoni.

Je, nikijaza namba yangu ya mtihani isiyokuwa ya NECTA, kwa mfano ya nje ya nchi, nitawezaje kuendelea kuomba mkopo?

  • Wakati  wa  kujisajili,  unatakiwa  kuchagua  kipengele  cha  ‘Non-NECTA students’ na kujaza kama inavyoelekezwa. Mfumo utakupatia namba ya  kidato  cha  nne  tofauti  na  ile  uliyojaza  ambayo  itatambuliwa  na mfumo wa Bodi. Namba hii mpya itatokana na taarifa yako ya namba uliyojazwa awali (isiyokuwa ya NECTA).

Inachukua muda gani fomu kufunguka baada ya kulipa?

  • Fomu inafunguka mara tu malipo yanapokamilika. Fomu inapochelewa kidogo  kufunguka,  mwombaji  unashauriwa  kutoka  (Sign  out)  na kujaribu kuingia tena (Sign in) katika mtandao ili aweze kuendelea na hatua zinazofuata.

Ikiwa nimelipa lakini sijapokea ujumbe wa kuendelea na maombi, nifanyeje?

  • Unatarajiwa kupokea ujumbe mara tu muamala unapokamilika. Ikiwa hautapata  ujumbe  ndani  ya  saa  moja  (dakika  60)  baada  ya  kufanya malipo, unashauriwa kuwasiliana nasi kwa namba ya simu +255 22 550 7910 au 0736 665 533 au barua pepe info@heslb.go.tz

Nitafanyaje ikiwa njia mojawapo ya kulipia mfano, CRDB, NMB, TPB, M-pesa, Airtel Money, Ezy Pesa, Tigo-Pesa, T-Pesa itanigomea kulipa na kuendelea?

  • Kwa kuwa kuna njia zaidi ya moja ya kulipia, unashauriwa kutumia njia ya  malipo  ambayo  ni  rahisi  kwako  au  inapatikana  sehemu  uliyopo wakati ukifanya malipo.

Nifanyeje iwapo nimesahau neno langu la siri (Password)?

  • Utapaswa  kubofya  kiunganishi  cha  “Forgotten  the  Password?”  na kisha utapata neno jipya la siri hapo hapo (kwenye screen) mtandaoni.

Je, ni wapi nitahakiki cheti za kuzaliwa au kifo cha mzazi?

  • Vyeti vya kuzaliwa na vya vifo vya wazazi lazima vihakikiwe na Wakala wa  Usajili,  Ufilisi  na  Udhamini  (RITA)  kabla  havijapakiwa  (uploaded) kwenye mtandao (olams)

Je kuna athari zozote ikiwa nimeambatanisha na kuwasilisha cheti ambacho hakijahakikiwa na RITA au Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar?

  • Ndiyo. Maombi yako yatakuwa hayajakamilika na hivyo kutofikiriwa katika hatua ya upangaji mikopo.
  • Unapaswa kuhakikisha nyaraka zote (siyo vyeti vya vifo au kuzaliwa tu) zinathibitishwa na mamlaka, taasisi au maafisa waliotajwa katika mwongozo.

Kama simfahamu mzazi wangu, nitajaza nini?

  • Unatakiwa  kujaza  taarifa  za  mlezi  au  mtu  mwingine  anayekulea  au kusimamia  masuala  yako  ya  Elimu.  Ni  lazima  taarifa  za  mlezi  au msimamizi  zithibitishwe  na  Serikali  ya  Mtaa  unakoishi.  Kama  mlezi anazo  nyaraka  rasmi  za  kukuasili  (adoption  document)  nazo ziambatanishwe.

Je, nikikosea kuchagua ‘Applicant’s Category’ natakiwa kufanya nini?

Ikiwa  bado  ‘huja-print’,  unaweza  kurekebisha  kwa  kurudi  kwenye kipengele  cha  ‘Applicant’s  Category’  na  kuchagua  kipengele  sahihi. Iwapo  umekamilisha  maombi  na  ku-print  fomu  yako,  unatakiwa kuandika  barua  ya  kuomba  kufanyiwa  marekebisho,  na  kuituma HESLB kwa njia ya EMS. Barua hiyo iwe na namba ya kidato cha nne yenye mwaka uliofanya mtihani huo.

Kama nina umri wa miaka 30, naweza kuomba mkopo?

  • Kwa  mwaka  wa  masomo  2019/2020,  umri  wa  juu  wa  mwombaji  ni miaka  33.  Umri  umeongezwa  ili  kuongeza  wigo  wa  wanufaika  wa mikopo.

Iwapo niliwahi kupata mkopo zamani na nikaacha, kushindwa au  kufukuzwa chuo, nitaweza kupata mkopo mwingine?

  • Iwapo  uliwahi  kuwa  mnufaika  wa  mkopo  wa  fedha  za  Serikali, utapaswa  kwanza  kurejesha  mkopo  wote  au  angalau  asilimia  25  ya deni  lako  kabla  ya  kufikiriwa  kupata  mkopo  mwingine.  Deni unalopaswa kulipa utalipata kwenye mtandao (screen) na utatakiwa kulipa kwanza kabla ya kuendelea na maombi ya mkopo mpya.

Kama nina wazazi wasio na uwezo, je niwasilishe uthibitisho wa aina gani ili kupata mkopo?

  • Mwombaji  ambaye  ana  mahitaji  maalum,  ni  lazima  mahitaji  na  hali yake ithibitishwe na mamlaka husika kama Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) au taasisi za aina hiyo. Taarifa za aina hii zitapekuliwa kuthibitishwa uhalisia na ukweli wake.

Kama nilikosa mkopo mwaka jana, nikalazimka kuahirisha masomo, natakiwa kuomba tena mkopo mwaka huu?

  • Unaruhusiwa  kuomba  upya  mkopo  mwaka  huu.  Maombi  yako yatapimwa  kwa  mwongozo  na  vigezo  vya  mwaka  2019/2020. Unashauriwa usome mwongozo kwa makini na kuuzingatia.
  • Aidha, kama unasoma mwaka wa pili au wa tatu na kuendelea na una uhitaji  wa  mkopo,  unaruhusiwa  kuomba  kwa  kuzingatia  vigezo  vya mwaka huu.

Nitafanyaje nisipoweza kumfikia mtoa huduma kwa njia ya Simu zinazoonyeshwa kwenye mtandao?

  • Kuna njia mbili za kuwafikia watoa huduma wa kitengo cha usaidizi  (Helpdesk) Njia ya kwanza ni kwa simu +255 22 550 7910 au 0736 665 533 na nyingine ni kwa barua pepe info@heslb.go.tz.
  • Unashauriwa  kuwasilisha  taarifa  au  changamoto  husika  kwa  njia  ya barua  pepe  ili  wataalamu  waifanyie  kazi  na  kukupigia  simu  kama itahitajika.  Kumbuka  kuandika  mawasiliano  yako  ya  simu itakayotumika kukupigia.

Je, nitajuaje kama nimejaza fomu ya maombi kwa ukamilifu?

Mwombaji una wajibu wa kuhakikisha nyaraka zote muhimu zimepakiwa kwenye mfumo wa maombi katika nakala laini. Nyaraka hizo ni pamoja na:
  1. Picha ya mwombaji na picha ya mdhamini wako;
  2. Vivuli vya nakala za vyeti vya kitaaluma zilizothibitishwa na Wakili au Mahakama;
  3. Vivuli vya nakala za vyeti vya kuzaliwa au kifo zilizothibitishwa na RITA;
  4. Nakala za barua za ufadhili kutoka katika taasisi zinazotambulika;
  5. Nakala ya kitambulisho cha mdhamini kilichothibitishwa na Wakili au Mahakama;
  6. Nakala ya fomu ya maombi iliyosainiwa na kugongwa muhuri na Serikali ya Mtaa, Mahakama au Wakili kama inavyoelekezwa;
  7. Aidha,  nakala  halisi  ya  fomu  ya  maombi  inapaswa  kusainiwa  na mwombaji na mdhamini wake
  8. Maelezo  ya  kina  yanapatikana  katika  mwongozo  uliopo  kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz)

Fomu za maombi ya Mikopo zinawasilishwaje Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu?

Baada  ya  kuzi-upload  na  kukamilisha  kujaza  fomu  ya  maombi, mwombaji a-print fomu iliyokamilika na kuituma kwenda kwa:
 Mkurugenzi Mtendaji,
 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu,
 Barabara ya Sam Nujoma – Mwenge
 S.L.P. 76068
 14113 DAR ES SALAAM

Je mwanafunzi anayekwenda kusoma ngazi ya Stashahada  (Diploma) anaweza kuomba mkopo?

  • Hapana. Wanafunzi wenye sifa za kujiunga na Stashahada hawana sifa za kuomba mkopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020.

Mwombaji atajuaje iwapo amepata mkopo?

  • Baada ya Bodi kupokea, kuhakiki na kuchambua maombi ya mikopo, majina ya Wanafunzi watakaofanikiwa kupangiwa mikopo yatatangazwa kupitia tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz) kabla ya kufunguliwa kwa vyuo vya elimu ya juu walikodahiliwa Wanafunzi husika.

Mkopo unatolewa kwenye vipengele (Loanable Items) vipi?

Kulingana na uhitaji, muombaji anaweza kupangiwa mkopo katika moja au baadhi ya vipengele vifuatavyo:
  • Chakula na malazi
  • Ada ya mafunzo
  • Vitabu na viandikwa
  • Mahitaji maalumu ya kitivo
  • Utafiti
  • Mafunzo kwa vitendo

Je, utaratibu wa kurejesha mkopo baada ya masomo ni upi?

  • Ni wajibu wa kila mnufaika wa mkopo kuhakikisha anarejesha mkopo baada ya kumaliza masomo. Maelezo ya utaratibu yanapatikana katika fomu uliyoombea mkopo. Hakikisha unayasoma kwa makini.

heslb - Bodi ya Mkopo>>Jinsi ya kufanya malipo baada ya kupata control number

Payment Instructions Using Vodacom Mpesa:    

  1. Dial *150*00#
  2. Select 4. Payments
  3. Select 5. Government Payment
  4. Select 1. Control Number
  5. Enter the Control number (e.g 991120000032)
  6. Enter Amount (e.g 30,000/=)
  7. Enter PIN
  8. Press 1 to Confirm:

Malekezo ya Jinsi ya kulipia kwa Vodacom Mpesa:

  1. Piga *150*00#
  2. Chagua 4. LIPA kwa M-Pesa
  3. Chagua 5. Malipo ya Serikali
  4. Chagua 1. Number ya Malipo
  5. Ingiza namba ya malipo (e.g 991120000032)
  6. Ingiza kiasi (e.g.30,000/=)
  7. Ingiza namba ya siri.
  8. Bonyeza 1 kuthibitisha

Wanafunzi waliyopewa mikopo 


Waliyopewa mikopo ya elimu ya juu mwaka wa masomo 2019/2020