NACTE SELECTION MARCH INTAKE 2020/2021

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAOMBI YA UDAHILI WA MACHI 2020 (MARCH INTAKE) KWA WAOMBAJI WA ASTASHAHADA NA STASHAHADA


nacte online selection

 Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)


Baraza linapenda kuufahamisha umma kuwa udahili wa wanafunzi katika ngazi ya Astashahada na Stashahada kwa kozi/programu zote isipokuwa Ualimu umefunguliwa rasmi kuanzia tarehe 15 Januari, 2020 na utakuwa wazi hadi tarehe 20 Februari, 2020. Hata hivyo, udahili wa Machi, 2020 (March Intake) hautahusisha programu za Afya kwenye vyuo vya Serikali.

Maombi ya kozi/ programu mbalimbali yatumwe moja kwa moja kwenye vyuo husika. Aidha Vyuo vitapokea maombi ya udahili na kufanya Uchaguzi kwa wanafunzi wenye sifa na kisha kuwasilisha NACTE majina ya waliochaguliwa kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuyatangaza. Vile vile Vyuo vinaelekezwa kuzingatia taratibu za udahili kama zilivyotolewa na Baraza katika mwaka wa masomo 2019/2020.

Baraza linawashauri Wahitimu wa Elimu ya Sekondari na Vyuo kwa ujumla kuhakikisha kuwa wanatuma maombi kwenye Vyuo vinavyokidhi ubora ambavyo vimeorodheshwa kwenye Kitabu cha Mwongozo wa Udahili kwa Mwaka wa Masomo 2019/2020 (Admission Guidebook for 2019/2020 Academic Year). Mwongozo wa Udahili unapatikana katika tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz). 



FORM FIVE SELECTION FOR ACADEMIC YEAR 2020/2021


Source:- nacte